Highlights

Waziri Duale asema kuwa serikali si lazima ishirikishe wananchi kuhusiana na ujenzi kituo cha Ebola Laikipia.

Na JB Nateleng

Waziri wa Afya, Adan Duale, amefika mbele ya wabunge kujibu maswali kuhusu utayari wa serikali katika kukabiliana na tishio la ugonjwa wa Ebola pamoja na mjadala unaoendelea kuhusu kituo cha karantini kilichopendekezwa eneo la Nanyuki, Kaunti ya Laikipia.

Duale amewaambia wabunge kuwa akiba ya vifaa vya kupimia na mavazi ya kujikinga (PPEs) iliyopo sasa inakadiriwa kutosheleza washukiwa takriban 220 wa awali endapo kutatokea maambukizi.

Amesisitiza kwamba serekali ipo ange kulinda wananchi dhidi ya ugonjwa huu wa Ebola.

Aidha, amesema serikali imeimarisha uchunguzi na ukaguzi katika vituo vyote vya kuingia nchini ili kudhibiti na kuzuia uwezekano wa kuingia kwa virusi vya Ebola.

Pia amesema kuwa sio lazima serekali iwahusishe wananchi kwenye ujenzi wa karantini ya ebola akitetea hatua hiyo kwa kusema kwamba ni hatua muhimu ambayo itasaidia nchi kujipanga ipasavyo kupambana na magonjwa kama vile Ebola.

Post Comment