Highlights

Wazee wa Kargi wahimizwa kuwa na simu kupokea fedha za Inua Jamii

Na Sabalua Moses

Wazee wenye umri wa miaka 70 na zaidi wanaojiandikisha katika mpango wa Inua Jamii eneo la Kargi wametakiwa kuwa na simu za mkononi ili waweze kupokea fedha zinazotolewa na serikali kupitia mpango huo.

Wito huo umetolewa na naibu chifu wa kata ndogo ya Kargi, Moses Itaanyua.

Akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu, Itaanyua amesema wazee wengi kutoka eneo la Kargi wamejitokeza kujiandikisha, jambo ambalo linaonyesha kuwa wameelewa umuhimu wa mpango huo unaolenga kuwasaidia kujikimu na kuboresha maisha yao.

Post Comment