Zoezi la usajili wa vitambulisho kuanza rasmi kesho eneo la Laisamis
Na Sabalua Moses
Wito umetolewa kwa wananchi kutoka Laisamis kutafuta vitambulisho katika zoezi litakaloanza hiyo kesho.
Akizungumza na shajara ya Radio Jangwani kwa njia ya simu chifu wa Laisamis Agostine Super amewataka wakazi kujitokeza katika zoezi hilo litakalo anza kesho na kuendelea kwa miezi mitatu zijazo.
Aidha, supeer amesema tayari serikali imetoa vitambulisho kwa wale waliotuma maombi huku zikisubiri kuchukuliwa.



Post Comment