Highlights

Lori la ngano lapinduka eneo la KBC Marsabit, watu wawili wakiponea na majeraha madogo.

Na Nyabande Orwa

Watu wawili wamejeruhiwa baada ya lori lililokuwa likisafirisha ngano kupinduka katika eneo la KBC, mjini Marsabit, adhuhuri ya leo.

Kwa mujibu wa polisi wa Marsabit, dereva wa lori hilo alisema kuwa gari lilipoteza mwelekeo kabla ya kupinduka kando ya barabara. Waliojeruhiwa ni dereva na utingo, ambao walipata majeraha madogo na kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Marsabit.

Polisi wameanzisha uchunguzi kubaini chanzo cha ajali hiyo. Tukio hili linajiri siku chache baada ya ajali nyingine kutokea katika eneo la Hula Hula kwenye barabara ya Marsabit–Moyale, ambapo mtu mmoja alipoteza maisha huku mwenzake akijeruhiwa.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment