County Updates, Diocese of Marsabit, Editorial, Local Bulletins, National News

KAMATI YA MAJI, MAZINGIRA NA ARDHI KATIKA BUNGE LA KAUNTI YA MARSABIT IMEITAKA SEREKALI YA KITAIFA KUITANGAZA HALI YA KUFURA KWA ZIWA TURKANA KUWA JANGA LA KITAIFA.

Na Isaac Waihenya & JB Nateleng,

Wawakilishi wadi hao wakiongozwa na MCA wa eneo la Loiyangalani Daniel Emojo na mwakilishi wadi mteule Daniela Lenatiyama wametaja kwamba wananchi wa eneo hilo wamekuwa wakihangaika tangu maji yalipoongezeka huku taasisi mbalimbali ikiwemo elimu zikiadhirika.

MaMCAs hao wametoa wito kwa serekali kuu kuweza kuingilia kati na kuwanasua wakazi ambao wameathirika pakubwa na kufura kwa ziwa hilo.

Wamekariri kuwa wananchi wa eneo hilo wamepata hasara kubwa kutokana na shule , kanisa na hata mali kusombwa na maji.

Watunga Sheria hao wa kaunti ya Marsabit wameitaka serekali kuingilia kati na kuwapa wavuvi msaada wa boti ili kuhakikisha kwamba wanaendelea kujimudu kimaisha.

Subscribe to eNewsletter