Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Pokonya Wananchi Wote Silaha Haramu – Askofu Dominic Kimengich Atoa Wito Kwa Serekali.

Askofu wa kanisa katoliki katika dayosisi ya Eldoret Dominic Kimengich.
Picha: Hisani

Na Isaac Waihenya,

Serekali imetakiwa kutwa silaha haramu zinazomilikiwa na wenyeji katika eneo la Keiyo Valley linalokumbwa na changamoto ya wizi wa mifugo ili Amani idumu katika sehemu hiyo.

Wito huo umetolewa na askofu wa kanisa katoliki katika dayosisi ya Eldoret Dominic Kimengich.

Akizungunza na vyombo vya habari Askofu Kimengich amesema kwamba itakuwa vyema iwapo serekali itapokonya wenyeji silaha haramu wanazomiliki kinyume cha sheria, ili kuhakikisha mizozo ya mara kwa mara ambayo hushuhudiwa katika eneo hilo inafika kikomo.

Aidha Askofu Kimengich amewataka viongozi wote katika eneo hilo kushirikiana kwa mambo ya Amani ili kuwezesha kuwepo kwa Amani na utulivu jambo analotaja kwamba litawaruhusu wananchi kuendelea na maisha yao bila matatizo.

Subscribe to eNewsletter