County Updates, Diocese of Marsabit, Editorial, Local Bulletins

MWANAME MMOJA KATIKA KAUNTI YA MARSABIT AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MWAKA MMOJA KWA KOSA LA KUHARIBU MALI YA DHAMANA YA SHILINGI 15,000.

Na Talaso Huka.

Mahakama ya Marsabit imemhukumu kifungo cha mwaka mmoja au bodi ya shilingi 100,000 mwanaume mwenye umri wa makamu kwa kosa la kuharibu mali ya dhamana ya shilingi 15,000.

Akitoa uamuzi huo hakimu Christine Wekesa amempata mstakiwa Hassan Duba na makosa ya kuharibu mali ya Dida Kara tarehe 10 mwezi wa mei mwaka wa 2022 katika kijiji cha Sagante eneo bunge la Saku, kaunti ya Marsabit.

Mahakama iliarifiwa kwamba mshukiwa Hassan Duba alifika nyumbani kwa Dida kara na kuharibu ua na kisha kutoweka.

Wakti uo huo Nura Adan Jillo amefungwa miaka tatu gerezani baada ya kupatikana na makosa ya kuiba ngamia katika eneo Shurr hapa jimboni Marsabit.

Mbele ya hakimu Christine Wekesa mshukiwa alikana mashtaka dhidi yake huku makama akimpa kifungo cha miaka mitatu gerezani bila bodi.

Subscribe to eNewsletter