Local Bulletins

WANAFUNZI WA NYAJANI MAARUFU INTERNS WANALIOFANYA KAZI KATIKA IDARA MBALIMBALI ZA SERIKALI YA KAUNTI YA MARSABIT KATI YA MWEZI SEPTEMBA MWAKA JANA 2023 HADI AGOSTI MWAKA HUU WALALAMIKIA KUTOLIPWA MISHAHARA YAO.

Na Isaac Waihenya,

Wanafunzi wa nyajani maarufu Interns wanaliofanya kazi katika idara mbalimbali za serikali ya kaunti ya Marsabit kati ya mwezi Septemba mwaka jana 2023 hadi Agosti mwaka huu wamelalamikia kutolipwa mishahara yao.

Wakiongozwa na Ismail Hirsi wafanyikazi hao wametaja kwamba walilipwa mishahara ya miezi minee pekee licha kufanya kazi katika kipindi cha mwaka mmoja.

Akizungumza na Radio Jangwani kwa njia ya Simu Hirsi ametaja kwamba ni jambo la kutamausha kuona kwamba wamejitolea na kufanya kazi yao kwa bidi ila serekali ya kaunti ya Marsabit imekosa kutimiza ahadi yao ya kuwalipa mishahara yao kama walivyokubaliana.

Mapema mwaka huu afisa mkuu katika idaya ya fedha na mipangilio Ahmed Yusuf aliwahakikishia wanafunzi hao kuwa watalipwa fedha zao zote kabla ya muda wao wa kuhudumu kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.

Subscribe to eNewsletter