WAUGUZI KATIKA KAUNTI YA MARSABIT WAMEAPA KUENDELEA NA MGOMO WAO HADI PALE SERIKALI YA KAUNTI YA MARSABIT ITAKAPOSHUGHULIKIA MATAKWA YAO YOTE.
September 19, 2024
Na Lelo Wako & Elias Jalle,
Vijana katika kaunti ya Marsabit wametakiwa kutumia wiki ya vijana kuonyesha talanta zao na vipaji walivyo navyo.
Wakiongozwa spika wa bunge la vijana Saku Youth Assembly Abdiaziz Boru, vijana hao wamewataka vijana wenzao kujiunga nao wiki ijayo katika wiki ya vijana ili kuonyesha vipaji na talaza zao kwa wanaMarsabit na hata ulimwengu kwa ujumla.
Abdiaziz Boru ametaja kwamba vijana wengi hapa jimboni wamelalia talanta zao huku akiitaja wiki ya vijana kama itayosaidia katika kuhakikisha kwamba vipaji walivyo navyo vinatambuliwa.
Kwa upande wake Halima Osman anayewakilisha watu wanaoishi na ulemavu amewahimiza vijana wanaoishi na ulemavu hapa jimboni Marsabit kutumia talanta zao kujiendeleza kimapato.