Local Bulletins

Wazazi wa Shule ya msingi ya Boru Haro waandaa dhifa ya kumpa kwaheri Mwalimu mkuu aliyepandishwa cheo

Na Grace Gumato

Wazazi, Walimu na kamati ya shule ya Boru Haro kaunti ya Marsabit Jumamosi hii wameandaa warsha katika shule hiyo ili kumpongeza mwalimu mkuu wa shule hiyo kwa kupandishwa ngazi na kupata cheo cha afisa mkuu wa kutathmini ubora wa elimu katika kaunti ndogo ya Loiyangalani.

Akizungumza katika warsha hiyo aliyekuwa mwalimu mkuu Wako Salesa ametoa shukrani za dhati kwa jamii ya eneo la Boru Haro akisema lazima shule hiyo iendelee kufanya vizuri hata kama mwalimu mkuu ameweza kupata kazi kwingine akisema shule hiyo inafaa kushirikiana vizuri na kamati na wazazi ili shule hiyo izidi kung’aa

Aidha walimu Hussein Guyo amempongeza walimu Wako kwa kuimarisha shule ya Boru Haro akisema kuwa alikuwa mwenye bidii katika kazi yake.

Wakaazi wa Boru Haro pia wameshukuru mwalimu Wako Salesa kwa kazi yake mzuri.

Subscribe to eNewsletter