SEREKALI YA KAUNTI YA MARSABIT YATAKIWA KUWAPIGA JEKI VIJANA NA WANAWAKE ILI KUPUNGUZA KIWANGO CHA UMASKINI.
October 17, 2024
Viongozi wa Marsabit wameshauriwa kuhamasisha umma kuhusu rasilimali asili zinazopatikana hapa jimboni. Viongozi katika kaunti ya Marsabit wameshauriwa kuhamasisha umma kuhusu rasilimali asili zinazopatikana hapa jimboni. Haya ni kwa mujibu wa mshauri wa Kiutawalawa shirika la NAPO Dr Elizabeth Pantoren Akizungumza na idhaa hii kwa njia ya kipekee Pantoren amesema[Read More…]
Kuna muda wa kila kitu ila huu ni muda wenu wa masomo. Ndio ushauri wa mtetezi wa haki za kinadamu katika kaunti ya Marsabit Nuria Golo kwa wasichana siku hii ya kusherekea siku ya mtoto msichana ulimwenguni. Akizungumza na Radio Jangwani ofisini mwake, Nuria amewataka wasichana kutumia muda huu kujiimarisha[Read More…]
Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya afya akili hii leo wafanyikazi katika kaunti ya Marsabit wametakiwa kulipa swala la afya ya akili kipau mbele wakiwa kazini mwao. Kwa mujibu wa afisa wa afya ya akili katika hospitali ya rufaa ya Marsabit Victor Karani ni kuwa kuna idadi kubwa ya wafanyikazi ambao[Read More…]
Wakaazi jimboni Marsabit wamezidi kuhimizwa kuasi tamaduni zilizopitwa na wakati kama vile wizi wa mifugo. Akizungumza na idhaa hii mapema leo asubuhi kwenye kipindi cha Amkia Jangwani, DCC wa Marsabit Central David Saruni amewataka wakaazi wanaoshirikiana na wahalifu haswa wanaotoka katika kaunti jirani kukoma. Ijumaa wiki jana watu waliokuwa wamejihami[Read More…]
Wito umetolewa kwa jamii ya Marsabit kutowaficha watoto waliona ulemavu na badala yake kuhakikisha kwamba wanapata haki zao za kimsingi. Kwa mujibu wa meneja wa kituo cha huduma Center mjini Marsabit Geoffrey Ochieng ni kuwa watoto waliona ulemavu wanafaa kupewa haki sawa za masomo na za kimaisha kama wenzao wasio[Read More…]
Na Isaac Waihenya & Abdilaziz Abdi, Wafanyikazi wa nyanjani CHPs katika kaunti ya Marsabit watalipwa mishara yao ya mwezi Julai, Agosti na Septemba hivi karibuni. Haya ni kwa mujibu wa mshirikishi wa huduma za jamii katika kaunti ya Marsabit Abdi Yusuf. Akizungumza na wahudumu wa afya hao wa nyanjani katika[Read More…]
Na JB Nateleng, Wito umetolewa kwa wahudumu wa afya katika kaunti ya Marsabit kufanya mazungumzo na serekali ya kaunti ili kumaliza mgomo ambao umeathiri sekta ya afya hapa jimboni. Akizungumza na idhaa hii kwa njia ya simu, Chifu wa lokesheni ya Kalacha Sabdio Wario amesema kuwa itakuwa ni afueni iwapo[Read More…]
Na Isaac Waihenya & Abdiaziz Abdi & Kame Wario, Wakaazi wa Marsabit wametoa hisia zao kuhusiana na uamuzi wa mahakama uliopiga marufuku hazina ya maeneo bunge nchini NG-CDF. Baadhi ya waliozungumza na Shajara ya Radio Jangwani wametaja kugadhabishwa na hatua hiyo ya mahakama ambayo wameitaja kama inayohujumu haki zao. Wametaja[Read More…]
Na JB Nateleng & Naima Abdullahi Wakazi wa Marsabit wametoa hisia zao kuhusiana na mgomo wa manesi ambao umeanza hii Leo kote nchini wakisema kuwa mgomo huu unahatarisha maisha ya wananchi ambao wanategemea huduma za afya kutoka kwa hospitali za umaa. Baadhi ya waliozungumza nasi wamesema kuwa mgomo wa manesi[Read More…]
NA NAIMA MOHAMMED Wito umetolewa kwa wananchi katika kaunti ya Marsabit kudumisha usafi ili kujizuia dhidi ya maradhi yanayotokana na uchafu. Kwa mujibu wa afisa anayesimamia maswala ya usafi katika kaunti ya Marsabit Chris Mabonga ni kuwa baadhi ya magonjwa ambayo yanaripotiwa hapa jimboni Marsabit yanaweza epukika iwapo wananchi watadumisha[Read More…]