Kaunti ya Marsabit kupata hospitali ya level six.
Na Nyabande Orwa
Rais William Ruto ametangaza mpango wa kujenga hospitali ya rufaa ya ngazi ya sita (Level 6) katika kaunti ya Marsabit kwa gharama ya shilingi bilioni 1.3.
Wakati uo huo rais Ruto amewarai wakazi wa kaunti hii kujiandikisha katika SHA kama njia moja ya kupokea huduma za afya pasi na kuwa na tatizo lolote.
Vile vile ametoa onyo kwa hospitali zinazoendelea kuwaitisha pesa Wakenya wanapofika hospitalini.



Post Comment