Highlights

Wataalam wa elimu Marsabit waunga mkono  wito wa rais kufadhili elimu ya juu.

Na Sabalua Moses

Siku chache baada ya rais William Ruto  kutoa mapendekezo ya  serikali kushughulikia ufadhili wa wanafunzi  wa vyuo vikuu. Wataalam wa elimu katika kaunti ya Marsabit wamesema kuwa  ikiwa mapendekezo hayo yatapitishwa na  bunge masomo ya  elimu ya juu yataboreka .

Kulingana na Profesa Chris Galgalo  na mtaaalam wa elimu  mapendekezo hayo yatasaidia kuboresha mfumo wa zamani ambao ulikuwa na changamoto chungu nzima.

Kwa upande wake Bedwin Kirimi ambaye ni  mtaalam wa  masomo katika chuo cha Tendo valley Marsabit amesema kuwa  nafasi  na mianya katika sekta ya elimu inafaa kujazwa  na mfumo wa sasa elimu ya juu  kuboreshwa .

Post Comment