County Updates, Editorial, Local Bulletins

WANANCHI JIMBONI MARSABIT WATAKIWA KUHAKIKISHA KWAMBA MAZINGIRA YANASALIA KUWA SAFI KWA KUZUIA KUTUPA CHUPA ZA PLASTIKI.

Na Isaac Waihenya,

Wananchi jimboni Marsabit wametakiwa kuhakikisha kwamba mazingira yanasalia kuwa safi kwa kuzuia kutupa chupa za plastiki.

Akizungumza na wananchi hapa mjini Marsabit mratibu wa maswala ya mazingira nchini Justus Nyamu ambaye yupo kwenye ziara ya mwezi mmoja hapa jimboni Marsabit ametaja kwamba chupa za plastiki zinachangia kwa asillimia kubwa kuharibu mazingira hapa jimboni.

Nyamu ametaja kwamba serekali imeaza kuwatunuku wanaotunza mazingira kwa kuokota chupa za plastiki na kuzitumia kwa njia mbadala huku akiwataka wananchi wa Marsabit haswa vijana kukumbatia zoezi hilo.

Aidha Nyamu amewaonya wale wanaoharibu mazingira kwa kuzichoma chupa hizo na hata kutumia karatasi za plastiki kuwa watachuliwa hatua kali kisheria.

Subscribe to eNewsletter