County Updates, Editorial, Local Bulletins, National News

MWANAUMME MMOJA AFUNGWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO GEREZANI BAADA YA KUPATIKANA NA KOSA LA KUMJANISI MTOTO WA MIAKA 7 KATIKA ENEO LA KIWANJA NDEGE,MARSABIT.

Na Talaso Huka,

Mwanaumme mmoja mwenye umri wa makamu   amefungwa kifungo cha miaka mitano gerezani baada ya kupatikana na kosa la kumjanisi mtoto wa miaka saba.

Mshukiwa Roba Godana Tura anadaiwa kwamba mnamo tarehe 2 mwezi wa mechi mwaka huu wa 2024 katika eneo la kiwanja ndege hapa mjini Marsabit alijaribu kumnajisi mtoto mwenye umri wa miaka saba.

Mshukiwa alifikishwa mbele ya hakimu Christine Wekesa na kukanaa mashtaki dhidi yake huku mahakama ikimpa kifungo cha miaka 5 gerezani.

Wakti huo uo Osama Guyo,Alberet Turumbeta na Abaya Merisk wamefikishwa katika Mahakama ya Marsabit kwa kosa la wizi.

Washukiwa hao wanadaiwa kuwa mnamo tarehe 21 na tarehe 23 mwezi wa Disemba mwaka wa 2023, katika kata ya Ilolo eneo la Illeret kaunti ndogo ya North Horr waliiba mali ya Ilolo Beach Management Unit, yenye dhamana ya shillingi 500,000.

Washukiwa hao wamefikishwa mbele ya hakimu Chrisine Wekesa huku kesi hiyo ikitarajiwa kutajwa tena hiyo kesho tarehe 19 mwezi Septemba mwaka huu wa 2024.

Subscribe to eNewsletter