County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Zoezi la kuwapiga msasa maafisa wa NPR katika kaunti ya Marsabit latarajiwa kuanza mwezi huu.

 

Kaimu kamishna wa kaunti ya Marsabit David Saruni.
Picha;Hisani

Na Isaac Waihenya

Idara ya usalama katika kaunti ya Marsabit itaaza zoezi la kuwapiga msasa watakaopewa nafasi za maafisa wa akiba yaani NPR mwishoni mwa mwezi huu wa Januari.

Zoezi hilo linatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Machi mwaka huu.

Kwa mujibu wa kaimu kamishna wa kaunti ya Marsabit David Saruni ni kuwa zoezi hilo litafanyika kwa ushirikiano na wananchi ili kuhakikisha kwamba wataokabidhiwa majukumu hayo ni watu waaminifu na watakao yatekeleza kwa ubora wake.

Kuhusiana na Video inayosambaa mitandaoni inayoonyesha wezi wa mifugo wakiwaiba mifugo usiku wa manane,Saruni ametaja kuwa uchunguzi tayari umeanzishwa ili kuwatia baroni wahalifu hao.

Aidha mkuu huyo wa usalama jimboni alitoa wito kwa wananchi kusitisha swala la wizi wa mifugo huku akiwaonya watakaopatikana wakiendeleza uhalifu huo.

Subscribe to eNewsletter