County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Jesca Anna Napoya aongoza katika shule ya upili ya Bishop Cavallera Girls kwa kupata gredi ya A- ya alama 74.

 

Jesca Anna Napoya aongoza katika shule ya upili ya Bishop Cavallera Girls kwa kupata gredi ya A- ya alama 74. Picha; Hisani

Na Isaac Waihenya Na Samuel Kosgei,

Jesca Anna Napoya kutoka shule ya upili ya Bishop Cavallera Girls ndiye aliyeongoza katika shule hiyo kwa kupata alama ya A- ya alama 74.

Wanafunzi 50 kati ya 52 wamefanikiwa kupata alama za kujiunga na chuo kikuu. Mwanafunzi mmoja alipata alama ya A, B+1, B 13, B- 19, C+ 16 na C 2 kwa wastani wamepata pointi jumla ya 7.9

Shule ya upili ya Manyatta Mixed moyale imenakili alama za wastani ya pointi 8.2 kutokana na kupata mwanafunzi 1 aliyepata alama ya A-, B+ 14, B 57, B- 79, C+ 25, C 5 na C-1

Shule ya wasichana ya Moi Girls hapa Marsabit imekua na pointi wastani ya 6.9 huku wanafunzi 117 wakipata alama wastani ya kujiunga na chuo kikuu.

Shule ya upili ya Rukesa imekua na B plain moja, B- 15, C+ 23 huku wanafunzi 49 wakifaulu kujiunga na chuo kikuu. Wanafunzi 59 wa shule ya sekondari ya Butiye Mixed Moyale pia wamefanikiwa kupata alama kujiunga na chuo kikuu.

Katika shule ya upili ya Chalbi High eneo bunge la NorthHorr, wanafunzi 22 kati ya 41 waliofanya mtihani wa KCSE mwaka jana wamefaulu kujiunga na chuo kikuu baada ya kupata gredi ya C plus kwenda juu.

Mwanafunzi bora katika shule hiyo ni Jillo Dokata aliyezoa gredi ya B- ya alama 57.

Aidha wanafunzi wananane wamezoa gredi ya B-, 14 wakiwa na C plus, 14 wakipata C na wanafunzi watano wakizoa gredi ya C-

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Molu Kala amesifia vijana wake kwa matokea bora, hii hapa sauti yake.

Katisha shule ya upili ya Moyale Boys wanafunzi 6 wamepata gredi ya B -, 11 wakipata C plus huku 10 wakizoa gredi ya C.

Subscribe to eNewsletter