County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Muungano wa wahubiri wa kanisa la PEFA Marsabit wawataka wakaazi kushirikiana na serikali ya kaunti ili kutafuta njia mwafaka ya kusuluhisha migogoro ya mara kwa mara.

Picha;Hisani

Na Irene Wamunda,

Muungano wa wahubiri wa kanisa la PEFA hapa Marsabit wamewataka wakaazi wa Marsabit kushirikiana na serikali ya kaunti ili kutafuta njia mwafaka ya kusuluhisha migogoro ya mara kwa mara baina ya jamii zinazoishi katika kaunti hii.

Wakizungumza na wanahabari kule Kanisani PEFA, Wahubiri hao wamekashifu vikali visa vya mauaji ambavyo vimekuwa vikiendelea katika kaunti ya Marsabit. Fredrick Gache Jibo ni Askofu wa kanisa PEFA Marsabit na pia kinara wa ushirika huo wa wahubiri.

Wamedokeza  kwamba hawatachoka kuendelea na mpango huu wa kuendelea kuhubiri amani kaunti hii ya marsabit,hasa kupitia kwa vyombo vya habari.

Subscribe to eNewsletter