County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Mwenyekiti Wa Chama Cha Wazazi Nchini Nicholas Maiyo Awashauri Wazazi Katika Kaunti Ya Marsabit Ambao Hawajawarejesha Watoto Wao Shuleni Kufanya Vile.

Mwenyekiti Wa Chama Cha Wazazi Humu Nchini Nicholas Maiyo. Picha; Hisani

By Adho Isacko Na Mark Dida

Mwenyekiti Wa Chama Cha Wazazi Humu Nchini Nicholas Maiyo Amewashauri Wazazi Kaunti Ya Marsabit Ambao Hawajawapeleka Watoto Wao Shuleni Kuhakikisha Wanafunzi Wanaripoti Shuleni Jinsi Walivyoagizwa.

Maiyo Amepongeza Wale Ambao Wameitikia Wito Wa Serikali Na Kurejesha Wanao Shuleni.

Kwa Mujibu Wa Maiyo, Kufikia Leo Ikiwa Ni Siku Ya Tatu Ya Kufunguliwa Kwa Shule Humu Nchini,Asilimia 58 Ya Wanafunzi  Katika Kaunti Ya Marsabit Wameripoti Shuleni.

Maiyo Ameyasema Hayo Alipokuwa Akikagua Shughuli Ya Watoto Kurejea Shuleni Katika Shule Ya Msingi Ya SKM Na St. Teresa Na Vilevile Shule Ya Upili Ya Dakabaricha Eneo Bunge La Saku.

Maiyo Amewataka Walimu Kuhakikisha Wanafunzi Wanavaa Ipasavyo Vibarakoa Ili Kuzuia Msambao Wa Ugonjwa Wa Corona.

Aidha, Ameeleza Kuwa Chama Cha Wazazi Kimeridhishwa Na Ufunguzi Wa Shule Kwani Watoto Walikuwa Hatarini Wakiwa Nyumbani Ikilinganishwa Na Wanapokuwa Shuleni.

Maiyo Amewataka Waalimu Walio Na Umri Na Miaka 58 Na Zaidi Na Pia Wanaokumbwa Na Matatizo Ya Kiafya Kusalia Nyumbani.

Subscribe to eNewsletter