County Updates, Local Bulletins

Mwanaume mmoja ahukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani kwa mashtaka ya wizi wa kimabavu na kumiliki silaha kinyume cha sheria.

By Grace Gumato,

Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 30 amehukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani kwa mashtaka ya wizi wa kimabavu na kumiliki silaha kinyume cha sheria.
Mshukiwa Ltaramatwa Lemangas alikamatwa tarehe 18 september, 2020 maeneo ya Namarei-Ngurunit kaunti ndogo ya Laisamis, ikidaiwa kuwa alisimamisha gari la kibinafsi na kuwatishia kwa bunduki waliokuwemo kwenye gari hilo kabla ya kuwaibia pesa kiasi kisichojulikana.
Lemangas alifikishwa mbele ya hakimu Tom Mbayaki Wafula ambapo alikanusha kuhusika kwenye uhalifu huo.
Mshukiwa ana haki ya kukataa rufaa ndani ya siku 14.

Subscribe to eNewsletter