County Updates, Local Bulletins

Maoni ya Wananchi mjini Marsabit kuhusiana na bajeti ya mwaka wa 2021/2022

Waziri wa fedha Ukur Yattani (wa pili kutoka kulia) wakati wa kusomwa kwa bajeti ya mwaka wa 2021/2022. Picha:Hisani

By Samson Guyo,

Huku bajeti ya kitaifa ikitarajiwa kusomwa alhamisi tarehe 10 mwezi huu,baadhi ya wananchi katika kaunti ya Marsabit wameelezea kusikitishwa na baadhi ya maswala yaliyopo kwenye bajeti.

Wakizungumza na idhaa hii wakaazi hao wamelalama kuwa mwaka nenda mwaka rudi matatizo yamekua yale yale kwa wananchi wa kawaida.

Aidha baadhi yao wameelezea kuwa iwapo serikali itaweka mfumo kabambe kupigana na ufujaji wa mali ya umma pamoja na kupunguza madeni kutoka kwa nchi za nje basi bajeti ikitangazwa huenda fedha hizo zikamfaidi mwananchi.

Subscribe to eNewsletter