County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Kaunti Ya Narok Yaongoza Kwa Asilimia 44 Ya Wanafunzi Walio Waliopata Ujawazito.

Picha; Hisani

By Mark Dida Na Adho Isacko

Kaunti Ya Narok Inaongoza Kwa Asilimia 44 Ya Wanafunzi Walio Walio pata Ujauzito Ikifuatwa Na Kilifi Kwa Asilimia 42.

Haya Ni Kwa Mujibu Wa Mwenyekiti Wa Chama Cha Wazazi Nchini Kenya Nicholas Maiyo Ambaye Amesema Kuwa Wote Waliotunga Wanafunzi Mimba Watakamatwa Na Kuadhibiwa.

Vile Vile Amesema Kuwa Wazazi Wote Ambao Hawajawapeleka Wanao Shuleni  Watachukuliwa hatua  kali Za kisheria.

Kulingana Na Maiyo, Baadhi Ya Wazazi Wakati Huu Wa Kupambana Na Janga La Korona Wameingiza Watoto Wao Kwenye Shughuli Za Vibarua, Huku Wasichana Wakiozwa Au Kukeketwa Hali Inayowafanya Kutorudi Shuleni.

Aidha Amewahimiza Wazazi Na Walimu Kuhakikisha Kuwa Hakuna Wageni Na Hata Wanahabari Wanaozuru Shule Kwa Sasa  Kuhakikisha Hakuna Mikusanyiko Ya Watu Shuleni Ili Kuzuia Maambukizi Ya Virusi Vya Corona.

Subscribe to eNewsletter