County Updates, Local Bulletins

Wanawake watekelezwa Marsabit na hata kufanyiwa uamuzi muhimu wakati wa majanga

Hafla ya kuratibisha namna ya kuwahamasisha wanawake kuhusu majanga ikiendelea  hii leo mjini Marsabit.
Picha;Radio Jangwani

Na Waihenya Isaac,

Jamii nyingi katika kaunti ya Marsabit zimewatelekeza wanawake huku wengi wao wakiumia kipindi kunapotokea majanga kwa kukosa ufahamu.

Haya yamebainishwa wakati wa hafla ya kuwahamasisha wanawake kuhusu namna ya kujimudu wakati wa majanga.

Afisa anayesimamia shughuli hiyo Sahara Ahmed amesema kuwa ipo hoja ya wanawake kupewa elimu na hamasa ya kutosha ili kuweza kujimudu kipindi cha majanga, ikizingatiwa kuwa wao ndio huathirika pakubwa wakati wa majanga.

Sahara Ahmed ameongeza kuwa muda mwingi wanawake hupangiwa maswala yanayowahusu kuliko kuhusishwa katika kuyapanga.

Hafla ya kuratibisha namna ya kuwahamasisha wanawake kuhusu majanga ikiendelea hii leo mjini Marsabit.
Picha;Radio JangwaniHafla hiyo iliyoongozwa na shirika la CIFA iliyaleta pamoja mashirika mengine kama vile Mwado, SAF na shirika la SND yanayotarajiwa kuandaa vikao vya hamasa kwa wanawake jimboni katika kaunti ndogo nne za kaunti hii.

 

Subscribe to eNewsletter