County Updates

Rais Kenyatta Atakiwa Kutatua Mizozo Ya Mara Kwa Mara Inavyoshuhidiwa Katika Maeneo Ya Kaskazini Mwa Nchi.

Picha; By Jillo Dida Jillo

By Jillo Dida Jillo

Vijana Kutoka Kaunti Za Marsabit Na Isiolo  Waliokutana Jijini Nairobi Wamemtaka Rais Uhuru Kenyatta Kuingilia  Kati  Na Kutatua Mizozo  Ya Mara Kwa Mara Inavyoshuhidiwa Katika  Maeneo Ya Kaskazini Mwa Nchi.

Katika Taarifa Yao Kwa Kiongozi Wa Taiafa, Vijana Hao Wakiongozwa Na Abdiaziz Boru Kutoka Kaunti Ya Marsabit Wamedokeza Kuwa Asasi Za Kiusalama Ambazo Zimejukumishwa Jukumu La Kulinda Amani Zimewatelekeza.

Wamemtaka Rais Uhuru Kenyatta Kutatua Swala Hilo Kabla Ya  Hatamu Yake Kukamilika.

Kwa Upande Wake Musa Boru Mwakilishi Wa Vijana Kutoka Kaunti Ya Isiolo Amelitaja Swala La Ugavi Wa Raslimali Kama Mojawapo Ya Swala Linalochangia Pakubwa Ukosefu Wa Usalama.

Amesema Kuwa Visa Vya Hivi Punde Vilivyotokea  Katika Eneo Qurri Ambapo Watu 6 Walipoteza Maisha Katika Vita Vya Kikakibila Vilisababishwa Na Mzozo Wa Raslimali.

Picha; By Jillo Dida Jillo

Amekariri Kuwa Ujenzi Wa Barabara Ya Isiolo Kuelekea  Mandera Kwenye Mradi Wa Mpango Wa Maendeleo Ya Kaskazini Na Kaskazini Mashariki Mwa Nchi (NEDI) Na Mradi Wa Ujenzi Wa Reli Ya Kisasa Inayokisiwa Kupitia Kaunti Ya Isiolo Ndicho Chanzo Kikuu Cha Vita Kati Ya Wakaazi Wanaoishi Mpakani Mwa Isiolo Na Wajir.

Abdi Osan Mwikilishi Kike Wa Katika Kundi Hilo La  Vijana Kutoka Kaunti Ya Marsabit Amesema Kuwa Umwagikaji Wa Damu Katika Ukanda Wa Kazkazini Mwa Kenya Umepitiliza Na  Kuwataka Viogozi Na Wakaazi  Wa Marsabit Kujumuika Kwa Mazungumzo Ili Kukomesha Uhuni Huo.

Subscribe to eNewsletter