County Updates, Local Bulletins

Makundi 15 Ya Wanawake Na Vijana Kutoka Kaunti Ya Marsabit Wamenufaika Na Shilingi Milioni 1.5

Mwakilishi Wa Kike Katika Kaunti Ya Marsabit Safia Shehk Adan Na Baadhi Ya Wananchi Wa Marsabit. Picha; Hisani

By Mark Dida.

Makundi 15 Ya Wanawake Na Vijana Kutoka Kaunti Ya Marsabit Wamenufaika Na Shilingi Milioni 1.5 Kutoka Kwa  Afisi Ya Mwakilishi Wa Wanawake Wa Marsabit Safia Shehk Adan.

Akiogoza Hafla Hiyo Kamishna Wa Kaunti Ya Marsabit Paul Rotich Amesema Kwa Makundi Hayo Sasa Yanaweza Kuendeleza Miradi Mbali Mbali Msimu Huu Wa Corona.

Vile Vile Rotich Amesisitiza Kuwa Msaada Huo Unaweza Ukaimarisha Na Kustawisha Uchumi Iwapo Pesa Hizo Zitatumika Kwa Njia Inayofaa.

Hata Hivyo Rotich  Amesema Kuwa Kaunti Ya Marsabit Ina Changamoto Za Kiusalama Zinazochochewa Na Watu Wachache Kutoka Baadhi Ya Jamii Za Marsabit.

Amewataka Wakaazi Kuchukua Jukumu La Binafsi Kueneza Njili Ya Amani Katika Kaunti Ya Marsabit.

Kwa Upande Wake Mbunge Wa Kaunti Safia Shehk Adan Ametaja Kuwa Mwaka Huu Afisi Yake Imeweza Kusaidia Makundi 90 Kutoka Sehemu Tofati Kaunti Ya Marsabit Akiongeza Kuwa Mwaka Ujao Ofisi Yake Inalenga Kutoa Msadaa Wa Karo Kwa Wanafunzi Shule Zitakapofugiliwa.

 

Subscribe to eNewsletter