Diocese of Marsabit, Editorial, Local Bulletins, National News

USALAMA WAIMARISHWA MPAKANI MWA KENYA NA ETHIOPIA BAADA YA KILIPUZI KUPATIKANA KATIKA ENEO LA BALES SARU KAUNTI NDOGO YA DUKANA KAUNTI YA MARSABIT.

Na JB Nateleng,

Usalama umeimarishwa  katika maeneo ya mpakani mwa Kenya na Ethiopia baada ya kilipuzi kupatikana katika eneo la Bales Saru kaunti ndogo ya dukana kaunti ya Marsabit.

Akizungumza na wanahabari DCC wa eneo la Dukana Njuki Nazarene amesema kuwa kilipuzi hicho kilipatikana na wafugaji ambao walikuwa wanaendelea na shughuli zao na kupiga ripoti kwa polisi ambao walifika eneo hilo na kuboresha usalama.

Njuki ameelezea kuwa waliweza kuwasiliana na maafisa wa jeshi kutoka idara ya ulinzi (KDF) ambao waliweza kutuma mtaalam wa kutegua kilipuzi hicho.

Subscribe to eNewsletter