Local Bulletins

JAMII IMETAKIWA KURIPOTI VISA VYOVYOTE VYA KUTILIWA SHAKA AMBAVYO VINAWEZA PELEKEA MAFUNZO YA ITIKADI KALI KATIKA KAUNTI YA MARSABIT.

Jamii imetakiwa kuripoti visa vyovyote vya kutiliwa shaka ambavyo vinaweza pelekea kuwepo kwa mafunzo ya itikadi kali katika kaunti ya Marsabit.

Kwa mujibu wa ACC wa Marsabit Central Martin Buluma ni kuwa jamii ifaa kuripoti visa vya watu kutoweka ili kuhakikisha kuwa idara ya usalama inafuatilia na kuzuia wao kupewa mafunzo ya itikadi kali.

Akizungumza ofisini mwake Buluma amewataka wananchi kuripoti viongozi wa kidini ambao wanatoa mafunzo yakupotosha jamii.

Aidha Buluma ametaja kwamba swala la kaunti ya Marsabit kuwa mpakani pia linaweza kuchangia visa hivi kwani watu wa tabaka mbalimbali wanatengamana.

Amekariri kuwa idara ya usalama imeweka mikakati kabambe kuhakikisha kwamba mafunzo ya itikadi kali kamwe hayafanyiki jimboni Marsabit.

Subscribe to eNewsletter