Wakazi wa Nyayoroad wapongeza ukarabati wa barabara, walalamikia kutelekezwa na serikali kuu
Na Joyce Akinyi & JB Nateleng
Wakazi wa eneo la Nyayoroad katika eneo bunge la Saku, kaunti ya Marsabit, wameeleza furaha yao kufuatia hatua ya serikali ya kaunti kuanza ukarabati wa barabara ya eneo hilo.
Wakizungumza na wanahabari, wakazi hao wamesema ukarabati huo ni nafuu kubwa kwao, kwani utarahisisha usafiri na kuchochea shughuli za kibiashara katika eneo lote la Marsabit Central.
Aidha, wameitaka serikali kuhakikisha kuwa kazi hiyo inakamilika kwa wakati ili kuwawezesha kuendelea na shughuli zao za kila siku bila changamoto.
Hata hivyo, wakazi hao wamelalamikia serikali kuu wakisema imekuwa ikiwatenga kimaendeleo kutokana na muda mrefu kuchukua bila kushughulikia ubovu wa barabara hiyo, licha ya kuwa ni muhimu kwa uchumi na maendeleo ya kaunti ya Marsabit.
Ikumbukwe kuwa wiki iliyopita, serikali ya kaunti ya Marsabit kupitia wizara ya barabara ilianzisha mradi wa ukarabati wa sehemu ya kilomita 2.5 ya barabara ya Nyayo, baada ya kuharibiwa vibaya na mvua kubwa zilizonyesha msimu uliopita.



Post Comment