Wakazi wa Badanrero walalamiki ukosefu wa maji
Na Sabalua Moses
Wakazi wa eneo la Bada Rero wamelalamikia ukosefu wa maji, hali ambayo imeathiri shughuli za nyumbani na ufugaji, na kuwafanya wakazi kutembea umbali mrefu kutafuta maji.
Wakizungumza na Radio Jangwani kupitia simu, baadhi ya wakazi wamesema changamoto ya maji imekuwa ya muda mrefu, na sasa inahitaji suluhisho la haraka kutoka kwa mamlaka husika.
Hata hivyo, chifu wa eneo hilo Dida Galgalo amesema kuwa kwa sasa hali iko shwari, akibainisha kuwa Bada Rero ina visima vya kutosha vinavyoweza kuhudumia wakazi wote endapo vitasimamiwa ipasavyo.



Post Comment