Wakazi Marsabit waeleza wasiwasi wao kufuatia maapendekezo ya karo ya shule za sekondari iongezwe.
Wakazi wa kaunti ya Marsabit wameeleza wasiwasi wao kufuatia mapendekezo ya walimu wakuu nchini ya kutaka karo ya shule za sekondari iongezwe.
Wakizungumza na Shajara, wakazi hao wamesema kuwa ongezeko hilo litawaathiri pakubwa wazazi wengi ambao tayari wanakabiliana na hali ngumu ya Maisha.
Baadhi yao wameeleza kuwa hatua hiyo inaweza pia kuchangia kuongezeka kwa visa vya uhalifu miongoni mwa vijana watakaoshindwa kuendelea na masomo na kubaki nyumbani bila shughuli za kufanya.



Post Comment