Loading Now

Highlights

Wachezaji 4,950 wasajiliwa kwenye FIFA Connect kuinua kiwango cha soka Marsabit.

NA JB Nateleng

Jumla ya wachezaji 4,950 kutoka Kaunti ya Marsabit wamesajiliwa katika mfumo wa FIFA Connect, hatua inayolenga kuimarisha na kuinua kiwango cha soka katika eneo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari, mwenyekiti wa shirikisho la soka Kenya (FKF) tawi la Marsabit, Godana Roba, amesema usajili huo utasaidia wachezaji kutambulika kimataifa, huku kila mchezaji akipewa namba maalum katika mfumo huo.

Godana pia amesema kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, shirikisho hilo limefanikiwa kutoa mafunzo kwa marefa na makocha ili kuboresha maendeleo ya soka jimboni.

Aidha, amewahimiza makocha kujitolea zaidi katika kutambua na kukuza vipaji vya vijana, akisisitiza kuwa kuna vipaji vingi vinavyohitaji kulelewa kwa uadilifu.

Pia ameahidi kuwa shirikisho hilo linaendelea na mipango ya kuhakikisha timu zote katika Kaunti ya Marsabit zinashiriki katika ligi ijayo.

Hata hivyo, Godana ametaja ukubwa wa kaunti ya Marsabit pamoja na changamoto za miundombinu kuwa kikwazo katika utekelezaji wa majukumu ya shirikisho hilo. Amesema licha ya changamoto hizo, ushirikiano kati ya viongozi, wachezaji na makocha ni muhimu ili kufanikisha usajili na ushiriki wa ligi.

Post Comment