Vijana Marsabit wahimizwa kukubali miito ya injili
NA JB Nateleng
Vijana katika katika kaunti ya Marsabit wamehimizwa kukubali miito ya kumtumikia Mwenyezi Mungu.
Akizungumza na Shajara Mseminaristi Mark Musungu Wanyama kutoka Shirika la Wamishonari la Comboni amewachangamoto vijana kujipa muda wa karibu na Mungu ili kutambua kusudi lao maishani.
Amesisitiza kuwa hili litachangia katika kujenga jamii yenye maadili mema.
Aidha, Mseminaristi huyo amewarai wazazi kuwalea vijana hao katika misingi ya imani ili kuwasaidia kutambua na kuthamini miito ya injili.
Leo Alhamisi Wanyama amepokea nadhiri ya daima na shirika la kimishonari la Comboni katika Parokia ya Kathedrali hapa Marsabit.

Jumamosi pia atatawazwa kuwa Shemasi katika misa itakayofanyika katika kanisa hilo.
Maafisa wa kliniki Marsabit waanza mgomo baada ya mazungumzo kugonga mwamba



Post Comment