Vijana 35 Marsabit wakamilisha tathmini ya TVET mashinani.
Na JB Nateleng
Shirika la Caritas Marsabit kwa ushirikiano na wakaguzi kutoka Nyeri National Polytechnic limeendesha tathmini ya mwisho kwa vijana 35 waliokuwa wakipata mafunzo chini ya mpango wa wezesha vijana TVET Mashinani.
Tathmini hiyo iliyofanyika katika maeneo ya Korr na Moyale imewapa washiriki hao nafasi ya kuonesha ujuzi waliopata katika kozi mbalimbali. Vijana waliokuwa Korr walitathminiwa katika ukarabati na ujuzi wa kutengeza pikipiki, huku wale wa Moyale wakitathminiwa kuhusu ujuzi wa oka Mikate na Keki.
Hatua hiyo inatarajiwa kuwawezesha vijana hao kupata vyeti vya kitaaluma na kuwapa uwezo wa kujiajiri, kupata ajira na kuanzisha shughuli za kiuchumi zitakazoboresha maisha yao.



Post Comment