Sport Bulletins

Liverpool yamsajili Luis Diaz kwa kima cha Euro milioni 60.

Mchezaji Luis Dias baada ya kujiunga na Brentford.
Picha;Hisani

Na Waihenya Isaac,

Klabu ya Liverpool imemsajili kiungo wa FC Porto ya Ureno Luis Diaz kwa kima cha Euro milioni 60.

Raia huyo wa Colombia ametia sahihi mkataba wa miaka mitano unusu na wekundu wa Anfield.

Kupitia ukurasa wao wa Twitter Liverpool imetaja kukamilika kwa uhamisho huo kama jambo lililosubiriwa kwa hamu na mashabiki wake.

Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amemsifia mchezaji huyo na kummiminia sifa tele tele.

Klopp alimtaja Luis Dias kama mchezaji bora na mchezaji ambaye klabu hiyo imekuwa ikiimfuatilia kwa muda mrefu.

Wakti uo huo klabu ya Brentford imemsajili mchezaji Christian Eriksen.

Eriksen amejiunga na Brentford kama mchezaji huria baada ya Inter Milan kukatiza mkataba wake mwanzoni mwa msimu huu.

Subscribe to eNewsletter