Sport Bulletins

Michuano Ya Kuwania Kombe La Ligi Kuu Nchini Uingereza Kuendelea Usiku Wa Leo.

Picha; Hisani

By Waihenya Isaac,

Michuano Ya Kuwania Kombe La Ligi Kuu Nchini Uingereza Inatarajiwa Kuendelea Usiku Wa Leo Huku Mechi Tano Zikiratibiwa Kugaragazwa.

Saa Tatu Usiku Burnley Ya Kocha Sean Dyche Itasaka Kuendeleza Matokeo Bora Mwaka Huu,Baada Ya Kushinda Mechi Mbili Za Mwisho Walizocheza,Itakapoikaribisha AstonVilla  Ugani Tuff Moor.

Aidha Chelsea Itaialika Wolvehamton Ya Kocha Nuno Espirato Santo Katika Uga Wao Wa Nyumbani Wa Stamford Bridge.

Mechi Hii Itakuwa Ya Kwanza Ya Kocha Thomas Tuchel Baada Yake Kukabidhiwa Mikoba Ya Kuinoa Ya Blues Baada Ya Kocha Franka Lampard Kupigwa Kalamu.

Aidha Saa Nne Unusu Usiku Brighton Itapambana Na Fulham Katika Ukoa Wa Amex Stadium Huku Timu Zote Z Mbili Zikingangana Kuondoka Katika Maeneo Hatari Ya Kushushwa Daraja.

Itimiapo Saa Tano Na Robo Usiku Vijana Wa Bredan Rodgers Leicester Watatafuta Nafasi Ya Kuchupa Hadi Katika Nafasi Ya Pili Ilikapotoana Kijasho Na Everton Uwanjani Goodison Park.

Mida Io Hiyo Manchester United Itasaka Nafasi Ya Kurejea Kileleni Mwa Jedwali La EPL Itakapovaana Na Sheffield United Uwajani Old Traford.

 

Subscribe to eNewsletter