Sport Bulletins

Michuano Ya Kuwania Kombe La Klabu Bingwa Barani Ulaya UEFA Champions League Awamu Ya 16 Bora Kurejelewa Usiku Wa Leo

Picha;Hisani

By Waihenya Isaac,

Michuano ya kuwania kombe la Klabu Bingwa barani ulaya   UEFA Champions league awamu ya 16 Bora inarejelewa  leo usiku huku mechi mbili zikiratibiwa kugaragazwa.

Bingwa wa mwaka wa 2019/2020 Liverpool atamenyana na RB Leipzig ya ujerumani jijini Budapest Nchini Hungary itimiapo saa tato usiku.

Mechi imelamika kuchezewa jiji Budapest Nchini Hungary baada ya Ujerumani kuzuia safari zozote za watu kutoka mataifa yanayoshuhudia ongezeko la maambukizi mapya ya virusi vya Korona, ikiwemo Uingereza.

Katika mechi nyingine itakayopigwa hii leo Bingwa mara 6 wa taji hilo Barcelona atatoana kijasho na Paris St Germain Katika uga wao wa nyumbani Camp Nou.

Mechi hii ilitarajiwa kumkutanisha Nyota wa Brazil Neymar Junior na klabu yake ya zamani Barcelona ila hatashiriki mechi hii kwa kuwa hakusafiri na kikosi cha Barca Kutoka na jeraha.

 

Subscribe to eNewsletter