Sport Bulletins

Gor Mahia Yatua Lusaka Zambia Ili Kuchuana Na NAPSA All Stars.

Picha;Hisani

By Waihenya Isaac,

Klabu ya Gor Mahia imetua mjini Lusaka Zambia, huku kikosi hicho kikitarajiwa kufanya mazozezi mepesi kabala ya mechi ya marudio kati yao na NAPSA All Stars ya Zambia Katika mchuano wa kufuzu kwa hatua ya makundi ya kombe la shirikisho  la soka barani Afrika CAF Confederation Cup.

Mechi hiyo Inatarajiwa kusakatwa katika uga wa National Heroes Stadium jijini Lusaka Zambia kuanzia saa kumi jioni.

Katika mechi ya mkumbo wa kwanza iliyopigwa Jumapili iliyopita, Gor walipoambulia kichapo cha goli moja kwa nunge Kutoka kwa  NAPSA All Stars ya Zambia katika mechi iliyogaragazwa Katika uwanja wa taifa wa Nyayo.

Mabingwa hao wa KPL sasa  watahitaji ushindi wa Magoli mawili kwa nunge ili kufuzu kwa hatua ya makundi ya kombe hilo kwa mara ya pili mtawalia.

Subscribe to eNewsletter