Mifugo 251 iliyoibwa Loiyangalani yarejeshwa
Na Caroline Waforo
Maafisa wa usalama wamefanikiwa kurejesha kondoo na mbuzi 251 waliokuwa wameibwa na washukiwa wa wizi wa mifugo katika kaunti ndogo ya Loiyangalani kaunti ya Marsabit.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Idara ya Polisi (NPS), maafisa walifuatilia mifugo hiyo hadi maeneo ya Lokilipi na Sarima, ambapo kulizuka majibizano ya risasi kati ya washukiwa waliokuwa na silaha na maafisa wa usalama.
Kutokana na makabailiano hayo washukiwa walitelekeza mifugo hiyo kabla ya kutoroka.
Mifugo yote 251 ipo chini ya ulinzi wa polisi ikisubiri kutambuliwa na kukabithiwa wamiliki wake halali.
Idara ya Polisi (NPS) imetoa onyo kali kwa wanaojihusisha na wizi wa mifugo, ikiahidi kuendelea kuwalinda wananchi na mali yao.



Post Comment