Highlights

Maonyesho ya sayansi na teknolojia  yafanyika katika Shule ya Don bosco Marsabit

Na Sabalua Moses

Maonyesho ya  kisayansi na teknolojia yameanza rasmi hii leo kwa siku tatu katika  taasisi ya elimu ya Don Bosco  ikijumuisha washikadau mbali mbali katika kaunti ya Marsabit .

 Akizungumza katika maonyesho hayo mkurugenzi mkuu  katika taasisi ya elimu ya Don bosco Fr Sunil Orathel amesema maonyesho hayo yatasaidia pakubwa katika mtaala wa CBE na kuhakikisha wanafunzi wanapata ujuzi wa kisayansi na teknolojia ya kisasa.

Vile vile padre Sunil amesema kupitia kwa taasisi za elimu za kiufundi vijana wanapata mafunzo yatakayo waendeleza kimaisha.

Kwa upande wake naibu mkurugenzi wa Don Bosco Samuel Mutiga amesema madhumuni ya maoonyesho hayo ni kuhakishisha kuwa ujuzi wa wanafunzi unatunzwa na kuelekezwa kwa njia itakayo wasaidia kimaisha.

Naye  David Malimo ambaye ni  mwanafunzi  katika chuo hicho anasema  maonyesho hayo yatasaidia wanafunzi kupata ujuzi na maarifa katika mtaala wa CBE.

Post Comment