Highlights

Hakimu wa Marsabit aonywa wananchi dhidi ya kutoa hongo ili kusaidiwa kupata bondi.

NA Samuel Kosgei

HAKIMU mkuu wa mahakama ya Marsabit Christine Wekesa ametahadharisha wananchi wanaosaka haki mahakamani dhidi ya kutoa hongo ili kusaidiwa kupata dhamana au bondi.

Hakimu Wekesa akizungumza na Radio Jangwani amesema kuwa kutoa pesa kwa mabroka ili kusaidiwa kupata bondi ni kuendeleza ufisadi kwa huduma ambayo mwananchi anafaa kupokea bure.

Anasema sera za mahakama hairuhusu suala la ufisadi, hivyo yeyote anayetoa pesa huwa amelaghaiwa na madalali wa mahakama.

Post Comment