County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins, National News

WALIOPATA UJAUZITO NA KUKATISHA MASOMO YAO WAREJESHWE SHULENI ILI WAENDELEE NA ELIMU. – ASEMA MKURUGENZI WA ELIMU, KAUNTI YA MARSABIT PETER MAGIRI.

Ni wakati wa kuasi mila potovu na kurusuhu wasichana katika kaunti ya Marsabit kusoma.

Haya yamekaririwa na mkurugenzi wa elimu katika kaunti ya Marsabit Peter Magiri.

Akizungumza katika eneo la Kalacha, wakati wa hafla ya wazee wa jamii ya Gabra kupiga marufuku tamaduni ya kuwaoza wasichana waliochini ya umri wa miaka 18, Magiri ametaja kwamba mila potovu zimewazuia wasichana kupata elimu na kuharibu maisha yao ya usoni.

Aidha Magiri ametoa wito kwa jamii kuwapeleka watoto wote shule bila kuwabagua.

Kadhalika mkurugenzi mkuu huyu wa elimu amewataka pia waliopata ujauzito na kukatisha masomo yao warejeshwe shuleni ili waendelee na elimu.

Subscribe to eNewsletter