County Updates, Diocese of Marsabit, Editorial, Local Bulletins, National News

WAFUGAJI KATIKA KAUNTI YA MARSABIT WAHIMIZWA KUHAMIA KATIKA MAENEO SALAMA KABLA YA MVUA INAYOTARAJIWA KUNYESHA.

Wafugaji katika kaunti ya Marsabit wamehimizwa kuhamia mahali salama wakati huu ambapo mvua inatarajiwa kunyesha katika sehemu mbali katika kaunti ya Marsabit.

Akizungumza na idhaa hii kwa njia ya simu mkurungezi wa mipango katika shirika la Pastrolist People Initiative (PPI) Stephen Baselle amesema kuwa wafugaji wasipojipanga mapema na kuhamia mahali salama basi wataweza kuadhirika na mafuriko iwapo yatashuhudiwa.

Hata hivyo Basele wamewarai wazazi na walezi kuwaepusha watoto wao na mila potovu kama vile ukeketaji na ndoa za mapema wakati huu ambapo shule zinatarajiwa kufungwa kwa likizo ndefu.

Subscribe to eNewsletter