County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins, National News

WAAKAZI WA MARSABIT WATOA HISIA ZAO KUHUSIANA NA MAPENDEKEZO YA BAADHI YA VIONGOZI WA KIDINI NCHINI KUTAKA MIRAA IPIGWE MARUFUKU.

Waakazi wa Marsabit wametoa hisia zao kuhusiana na mapendekezo ya baadhi ya viongozi wa kidini ya kupigwa marufuku utumiaji wa miraa hapa nchini.

Baadhi ya waliozungumza na Shajara ya Radio Jangwani kwa njia kipekee wameitaja hatua ya kupiga marufuku zao hilo kama itakayo wakandamiza wanaotegemea biashara ya miraa kama kitega uchumi chao.

Aidha, wamelitaja zao hilo kama lisilo na madhara kama inavyoashiriwa na baadhi ya watu wanaotaka zao hilo kupigwa marufuku.

Hata hivyo baadhi ya wakaazi wanaunga mkono kauli ya kupigwa marufuku kwa miraa, wakisema kuwa miraa inapoteza pesa na wakati kwa watumiaji.

Subscribe to eNewsletter