County Updates, Diocese of Marsabit, Editorial, Local Bulletins, National News

MWANAUMME MMOJA MWENYE UMRI WA MAKAMU ASHTAKIWA KWA KOSA LA WIZI WA SHILINGI MILIONI 1.6

Na Talaso Huka & Abdilaziz Abdi,

Mwanaumme mmoja mwenye umri wa makamu amefikishwa mbele ya mahakama ya Marsabit kwa kosa la wizi.

Mahakama imearifiwa kuwa mshukiwa Galgallo Boru Dida ambaye ni agenti wa chama cha ushirika cha shirika la FH la kati ya mwezi oktoba mwaka wa 2017 na Septemba mwaka wa 2023, aliiba mali ya Hawo Dida yenye dhamani ya shilingi 1.6 katika eneo la Loiyangalani kaunti ya Marsabit.

Mbele ya hakimu Christine Wekesa mshukiwa amekana mashtaka dhidi yake huku akiachilwa kwa bondi shillingi 1,000,000 au shillingi 200,000 pesa taslim.

Wakti ou huo mshukiwa Lowoi Ekal amefikishwa katika mahakama ya Marsabit kwa kosa la kumpiga na kuumiza Daniel Korobe.

Mshukiwa Lowoi Ekal amefikishwa mbele ya hakimu Christine Wekesa na kukubali mashtaka dhidi yake huku mahakama ikimwachilia na bondi ya shillingi 50,000 au shillingi 20,000 pesa taslim.

Subscribe to eNewsletter