County Updates, Diocese of Marsabit, Editorial, Local Bulletins, National News

IDARA YA ELIMU KAUNTI YA MARSABIT KUHAMISHA SHULE MSINGI YA EL MOLO BAY KATIKA MAENEO SALAMA.

Na JB Nateleng & Isaac Waihenya

Idara ya elimu katika kaunti ya Marsabit imesema kuwa shule msingi ya El Molo bay iliyo katika wadi ya Loiyangalani kaunti ya Marsabit itahamishwa hivi karibuni.

Haya ni kulingana na mkrugenzi wa elimu jimboni Marsabit Peter Magiri.

Akizungumza na idhaa hii kwa njia ya kipekee, Magiri ameelezea kuwa jamii ya Loiyangali imetoa ardhi ambapo  shule hiyo pamoja na wakazi wanaweza kuhamia mbali na ziwa Turkana.

Magiri ameirai serekali ya kaunti, pamoja na serekali kuu kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserekali kusaidia katika kuhakikisha kuwa shule hiyo imeweza kuhamishwa na kujengwa upya.

Na huku mtihani wa KAPSEA ikitarajiwa kuanza mwezi ujao mkuu huyo wa elimu jimboni amesema kuwa idara yake itahakikisha kuwa wanafunzi wa shule hizo wanakalia mtihani huo.

Subscribe to eNewsletter