Wakaazi wa Marsabit wakerwa na hatua ya kuahirishwa kwa vikao vya kutoa maoni bila kujulishwa mapema.
February 20, 2025
Na Sabalua Moses
Msimamizi mkuu anayesimamia maswala ya watoto katika kaunti ya marsabit Mukanzi Leakey ametoa himizo kwa wazazi pamoja na washikadau katika kaunti ya marsabit kuwa makinifu katika kutoa udhibiti kwa watoto wao wanapotumia mitandao ya kijamii.
Leakey amesema ijapokua wakaazi katika sehemu nyingi katika kaunti ya Marsabit bado hawana simu za rununu za kuingia kwenye mitandao bado kuna hatari ya watoto kujihusisha katika mambo ya ngono na ulanguzi wa watoto wanapotumia mitandao ya kijamii.
Vile vile Mukanzi amesema kuwa kuna hatari ya watoto kutumia mitandao bila udhibiti na kwa sasa amewahimiza washikadau mbali mbali pamoja na jamii kushirikiana pamoja kuripoti visa ambavyo vinahatarisha watoto katika mitandao kaunti ya Marsabit .
Pia amesema ni sharti washikadau wote katika kaunti ya Marsabit washirikiane kwa pamoja ili kutoa udhibiti mwafaka kwani watoto wapo katika hatari ya ulanguzi .