Local Bulletins

Mwanafunzi wa shule ya msingi azirai na kufariki baadaye alipokuwa akielekea shuleni kaunti ya Marsabit.

 Na Henry Khoyan

Mwanafunzi mmoja wa Shule ya Msingi ya Karare ameaga dunia ghafla leo Alhamisi alipokuwa akielekea shuleni na wenzake.

Chifu wa eneo hilo, Magdalene Ilimo, amedhibitisha kuwa mtoto huyo mwenye umri wa miaka 14 alizirai ghafla walipokuwa barabarani kuelekea shuleni na wenzake.

Wenzake walikimbia nyumbani kutoa ripoti ya tukio hilo. Chifu amesema mwanafunzi huyo alifariki alipofikishwa Hospitali ya Rufaa ya Marsabit.

 

Subscribe to eNewsletter