Local Bulletins

WATOTO 10 WALIODAIWA KUTEKWA NYARA MWANZONI MWA MWAKA HUU NA MHUBIRI MOJA KATIKA ENEO LA PARKISHON KAUNTI YA MARSABIT WAREJESHWA KWA FAMILIA ZAO.

Na Carol Waforo,

Watoto 10 waliodaiwa kutekwa nyara mwanzoni mwa mwaka huu na mhubiri moja katika eneo la Parkishon kaunti ya Marsabit wamerejeshwa kwa familia zao.

Akizungumza na shajara ya Radio Jangwani kwa njia ya simu afisa wa watoto hapa katika eneo bunge la Saku Medina Doko amesema kuwa watoto hao waunganishwa na wazazi wao hapo jana katika zoezi lililosimamiwa shirika la Child Welfare society of Kenya.

Medina amesema kuwa watoto 8 kati ya kumi watarejea mjini Nairobi ambapo wataendelea na elimu yao wakati shule zitakapofunguliwa kwa ufadhili wa shirika hilo.

Medina anasema kuwa watoto hao wapo mikononi salama.

Na huku shule zikisalia kufungwa kwa ajili ya likizo ya muhula wa pili afisa huyu wa watoto amewataka wazazi kujukumika katika malezi ya wanao ili kuwaepusha na mila potovu na tamaduni zilizopitwa na wakati.

Subscribe to eNewsletter