Local Bulletins

WAKAAZI WA MARSABIT WATOA HISIA ZAO KUHUSIANA NA UAMUZI WA MAHAKAMA ULIOPIGA MARUFUKU HAZINA YA MAENEO BUNGE NCHINI NG-CDF

Na Isaac Waihenya & Abdiaziz Abdi & Kame Wario,

Wakaazi wa Marsabit wametoa hisia zao kuhusiana na uamuzi wa mahakama uliopiga marufuku hazina ya maeneo bunge nchini NG-CDF.

Baadhi ya waliozungumza na Shajara ya Radio Jangwani wametaja kugadhabishwa na hatua hiyo ya mahakama ambayo wameitaja kama inayohujumu haki zao.

Wametaja kuwa kutupiliwa mbali kwa hazina hiyo kutachangia watoto kutoka familia zisizojiweza kushindwa kuendelea na elimu kutokana na wazazi kushindwa kumudu gharama ya juu ya elimu.

Aidha wameitaka mahakama kuangazia upya uamuzi huo kuhusiana na hazina hiyo kwani utaadhiri hatua zilizopigwa katika kuimarisha kiwango cha elimu hapa nchini.

Subscribe to eNewsletter