Local Bulletins

WAKAAZI WA MARSABIT WATOA HISIA ZAO KUHUSIANA NA KIONGOZI WA WIPER KALONZO MUSYOKA KUWA KINARA WA UPINZANI NCHINI.

Na Ebinet Apiyo,

Baada ya kinara wa upinzani nchini Raila Odinga kuonekana kufanya kazi na serekali na baadhi ya wanachama wa ODM kuteuliwa kama mawaziri, wakaazi wa kaunti ya Marsabit wametoa hisia zao kuhusiana na iwapo kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka anatosha kushikilia wadhifa wa kinara wa upinzani nchini.

Baadhi ya waliozungumza na idhaa hii wamelitia shaka ufaafu wa Kalonzo kuwa kinara wa upinzani wakisema kwamba hana ushawishi wakutosha hata katika eneo anakotoka.

Wengine wao wamelalamikia kile wamekitaja kuwa ni ukosefu wa msimamo dhabiti katika kushughulikia mambo mbalimbali.

Aidha baadhi yao wamemtaja Kalonzo kama mtu pekee aliyesalia na ambaye anauwezo wa kushikilia wadhifa huo haswa kuzingatia viongozi wengine katika muungano wa Azimio.

Subscribe to eNewsletter